Maumivu makali ya hedhi “severe painful periods


 
Maumivu makali sana ya hedhi “severe painful periods

Maumivu yanatokea wakati wa hedhi ila kwa wengine maumivu haya yanakuwa makali sana kiasi cha kuharibu mpangilio wa maisha yako ya kila siku changamoto hii imezidi kuongezeka na kibaya zaidi ni kwamba wengi wanapopitia changamoto hii wanatafuta suluhisho la haraka matumizi ya vidonge kama vile ibuprofein kwa muda mrefu yanaweza kuwa na athari  nyingine kama kuumwa kichwa  na mara nyingi matumizi ya dawa kiholela yanaweza yakaonekana kuleta unafuu kwa muda mfupi ila tatizo linakuwa bado halijatatuliwa kabisa ni muhimu kuelewa hali hii inazidi kuwa ngumu zaidi kwa kuelewa haya inaweza kusaidia angalau kutatua

Baadhi ya mbinu hizi zinaweza kuleta unafuu 

  1. Sababu ya kwanza ni upungufu wa virutubisho katika vyakula ambavyo vinatumika kwa wingi

Virutubisho kama vile magnesium husaidia na omega -3 husaidia sana kupumzisha misuli na kupunguza “inflammation” na kupunguza uzalishwaji wa kemikali ambazo zinaweza kusababisha ongezeko zaidi la maumivu

Unadhani nini kitatokea ukivikosa hivi?

Katika moja ya utaifi uliochapishwa na “National institute of health (NIH)” wanawake wa umri kati ya miaka (18-22) waliokuwa wakipitia maumivu ya hedhi walisimamiwa kutumia virutubisho vya omega-3 kwa muda wa miezi mitatu matokeo yake ni kwamba wale waliofanya hivyo hawakuhitaji dose kubwa ya ibuprofen na matumizi hayo yalipunguza ukali wa maumivu.tafiti zilionyesha matokeo hayo pia kwa magnesium

 Hivyo jitahidi kuhakikisha mlo wako una vyakula ambavyo vinakupa virutubisho vya kutosha

Unavipata wapi ? katika mboga mboga za majani kwa wingi,Samaki,almonds,chia seeds,parachichi hakikisha unakula mlo kamili

  1. Vyakula vya kisasa

Vingi utakuta kwamba vina vitu ambavyo vinachochea zaidi “inflammation” huvuruga afya ya tumbo lako “gut health” hasa husababisha kupotea kwa jamii ya bacteria waitwao “estrobolome” ambao wanahusika na kuchakata na kusaidia kuondoa estrogen mwilini hivyo kuleta balance

vyakula vyenye sukari nyingi vinajulikana kwa kuchochea zaidi "inflammation" na dawa kama vile ibuprofen ambayo hutumiwa na wengi kipindi hiki inasaidia kupunguza maumivu hayo kwani ni "anti inflammatory' yaani ianapambana na inflammation hivyo ukipunguza ulaji wa vitu vyenye sukari nyingi  utapunguza inflammation na maumivu pia yanaweza yakapungua

Unafikiri nini kitatokea wakipotea hao?

Mchakato huo hautafanyika kwa ufanisi kinachofata ni kwamba viwango vya estrogen mwilini vinakuwa vikubwa zaidi “estrogen excess” na kupelekea maumivu kuwa makali zaidi au kuendelea kwa muda mrefu zaidi

 

  1. Kukosa mazoezi pia kunachangia

Swala la mazoezi ni changamoto kwa wanawake kutokana na baadhi ya fikra ambazo tayari wameshajijengea hivyo wengi hawafanyi mazoezi jambo ambalo linaongeza hatari zaidi mazoezi yanasaidia sana katika kuhakikisha “hormone balance” hasa yanasaidia balance katika homoni ya estrogen ,kupunguza “inflammation” na pia husaidia kupunguza maumivu ya hedhi

Mazoezi unayoyaepuka yanaweza kukusaidia sana.

Katika moja ya tafiti watu 1808 waliomaumivu yalionekana kupungua kutokana na ufanyaji wa mazoezi ,mazoezi yalionekana ni njia nzuri sana ya kupunguza maumivu kipindi cha hedhi

rejea chapisho halisi la utafiti huo (national institute of health)

Matokeo ya namna hiyo yameonekana katika tafiti zingine nyingi sana

mazoezi yanasaidia kwanza ni kwasababu yanapunguza inflammation na kuziweka homoni katika utaratibu sahihi

 

Je utaanza kufanya mazoezi?

Namna rahisi za kuanza kufanya mazoezi ni kuanza tenga muda wa kufanya mazoezi,tembea,ruka kamba jizoeshe yatakusaidia kukuweka sawa kimwili na kiakili pia

  1. Msongo mkali wa Mawazo “chronic stress”

Msongo mkali wa Mawazo “chronic stress” ni moja kati ya wavurugaji wakuu wa “hormone balance”  ongezeko la homoni za stress husababisha homoni zingine kama progesterone zisiweze kufanya kazi vizuri hivyo hupelekea maumivu makali zaidi “intense contraction and painful scramps”

  1. Shida katika ini "liver problems"

Ini linahusika katika kuchakata homoni zifanye kazi kwa ufanisi zaidi nini kitatokea kama kazi hiyo haifanyiki vizuri?

Yanayoweza kuathiri utendaji kazi wa ini ni vitu kama vile pombe,utegemezi wa madawa,na sumu mbalimbali

Ini litashindwa kuchakata homoni kama “estrogen” kwa ufanisi na kuhakikisha kwamba ipo kwa kiwango sahihi hivyo homoni hiyo huwa nyingi na kupelekea maumivu kuwa makali zaidi

  1. Sababu nyingine ni “endocrine disruptors” kemikali ambazo zinajificha katika baadhi ya vitu ambavyo tunavitumia kila siku iwe nim aji,vyakula,bidhaa za urembo

 Baadhi ni kama

Bisphenol A (BPA): Inatumika kwenye plastiki na mipako ya ndani ya baadhi

Phthalates: Inapatikana kwenye plastiki, vifungashio vya chakula, na bidhaa za kujipamba.

Dawa za kuua wadudu: Kama vile DDT, atrazine, na chlorpyrifos.

Sikuwahi kulichukulia swala hili kwa uzito zaidi hadi pale nilipokutana na kichwa cha Habari katika gazeti la mwananchi “Chembe za plastiki zinaathiri ubora wa mbegu za kiume” Habari hii ilielezwa na Profesa Mohamed Janabi ambaye ni mkurugenzi wa hospitali ya taifa Muhimbili alieleza kwa undani namna ambavyo kemikali kama vile BPA ambayo inatumika katika kutengeneza plastiki na inatumika katika vyombo vya chakula kama ulivyoona hapo juu na namna ambavyo zina athari katika afya ya uzazi na kuoenekana kama jambo ambalo linachangia baadhi ya matatizo katika afya ya uzazi

Kwanini zinaleta athari hizi?

Kemikali hizi zinafanya kazi kama homoni za mwili hivyo zinaweza kuharibu utaratibu wa kawaida au kupelekea ongezeko la baadhi ya homoni Fulani na kupungua kwa nyingine hivyo hupelekea maumivu makali kwa mwanamke

Jitahidi kupata ushauri wa daktari unapopitia hali hii tafuta msaada na ushauri wa kitaalamu utapata dawa na kushauriwa nini cha kufanya pia

 


Health Talks... Welcome to WhatsApp chat
Howdy! How can we help you today?
Type here...