Dalili za ukinzani wa insulin
Jambo moja ambalo unaweza ukalifanya leo ni kuhakikisha
unaichunguza afya yako ili kujua kinachoendelea mwilini mwako kwani ni wengi
wana hali hii tayari ila hawajui sana kwa sababu hali hii huendelea taratibu na
mwishowe hali hii hupevuka na kuingia katika matatizo halisi kama kisukari na
magonjwa mengine sugu vishairia vyake ni kama vifuatavyo
1.Kiwango cha insulin ya zaidi ya sita yaani 6uU/ml katika
kipimo cha maabara
2.Kipimo cha kiuno “waist circumference” kwa wanaume upana
wa kiuno zaidi ya inchi 40 na wanawake upana wa kiuno wa inchi 35 ni kiashairia
kuwa tayari mtu anapitia hali ya ukinzani wa insulin sana kwa sababu mafuta
mengi katika eneo hili yanajulikana kuchangia ukinzani wa insulin
3.Shinikizo la juu la damu ,kipimo zaidi ya 140/90 mmHg
pia ni dalili ya ukinzani wa insulin
4.Wanaotumia pia dawa za kupunguza shinikizo la juu la damu
ni dalili ya wazi kabisa kwamba kuna ukinzani wa insulin
5.Wingi wa sukari zaidi ya 100mg/dl ni dalili pia ya kuwa na
tatizo hili la ukinzani wa insulin mwilini
6.Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa yaani libido ndogo na kwa
wanaume kukosa nguvu za kiume japo sio muda wote ila nacho ni kishiria cha
ukinzani wa insulin
7.Dalili zingine ni kama vile kushindwa kulala “insomnia”
kupanda na kushuka kwa nguvu za mwili ,,kuhisi kuchoka sana baada ya kula,maumivu
ya magoti na viungo KUMBUKA hizi dalili
zinaweza kuwa ni kutokana na tatizo lingine na isiwe ukinzani wa insulin cha
muhimu ni kujua chanzo cha dalili hizi ni nini
8.Matatizo katika homoni kama vile PCOS yaani polycystic
ovarian syndrome
Kama nilivyotangualia kusema hapo mwanzo inabidi tuwe na
mkakati wa kuchunguza na kujua hali zetu za kiafya kumbuka inachukua miaka hadi
10 kutoka ukinzani wa insulin hadi kuona mtu ana kisukari
Join the conversation