sehemu ya pili
SEHEMU YA PILI
7. THEY DON’T MAKE THE SAME MISTAKES OVER AND OVER & THEY DON’T GIVE UP AFTER THE FIRST FAILURE
Tafsiri yake :Hawarudii makosa yale yale kila mara na pia hawakati tamaa baada yakushindwa mwanzoni
The only real mistake is the one from which we learn nothing. -JOHN POWELL
kuhusu makosa mwandishi anasema kitakachosaidia ni
kukiri kwamba tumekosa
kuangalia namna ya kutokurudia kosa kuelewa mambo yaliyotufanya tukosee na kuyaepuka huko mbeleni
kuhusu makosa mambo haya hayawezi kusaidia
kuleta visingizio vya kwanini umekosa au kukataa kukiri kosa lenyewe
kujiweka katika nafasi ya kukosea na kujifanya kwamba tunaweza kushinda majaribu na mwsihowe unakosea tena
Kuhusu makosa tunapaswa kukubali ukweli huu kwamba ukiangalia mara nyingi ambapo ulijitetea sana kuhusu jambo fulani ukitulia na kuwaza vizuri utagundua kwamba ulikuwa unahusika ila ulitumia visingizio kukimbia majukumu
8. THEY DON’T RESENT OTHER PEOPLE’S SUCCESS
Tafsiri yake : Hawaonei wivu mafanikio ya watu wengine/Hawachukii kufanikiwa kwa wengine.
Mwandishi anamnukuu Nelson Mandela "Resentment is like drinking poison and then hoping it will kill your enemies"
kwamba kufanya hivyo ni kama kunywa sumu na kutegemea kwamba itamuua adui yako
mwandishi ameweka wazi kwamba jealous ni kusema “I want what you have,” nataka ulichonacho na resentment ni kusema kwamba nataka ulichonacho na sitaki wewe uwe nacho
je moja wapo ya sifa hii inaonekana kwako? unajilinganisha kila mara (hadhi yako,vitu,muonekano) na watu wengine? ni ngumu kwako kuweza kuwasikiliza wenzako wakielezea mafanikio yao? unahofu kwamba wenzako watakuona kama mpotezaji/uliyefeli "loser"? unaona aibu juu ya kukosa kwako mafanikio?
kwanini tunajifananisha na watu wengine? ni swali la kujiuliza
Kujifananisha kila mara kunaweza kukuletea hisia za kutokutosheleka na kukosa amani ya ndani na kunasababisha wakati mwingine kuwa na hasira juu ya wengine
Ni muhimu kujifunza kufurahia matokeo ya wengine na mafanikio yao na kujifunza toka kwao
9. THEY DON’T FEAR ALONE TIME
All man’s miseries derive from not being able to sit quietly in a room alone. —BLAISE PASCAL
Tunaishi katika kipindi ambacho tunaogopa kuwa peke yetu (kumbuka upo utofauti kati ya kuwa peke yako na kuwa mpweke)
kila wakati tupo mtandaoni wengi wanapitia hofu ambayo imepewa jina la FOMO -fear of missing out kwamba tunaogopa kupotea mtandaoni
unaweza ukabisha kwamba huna FOMO lakini ili uielewe FOMO ni kile ambacho kinatokea simu yako inapokaribia kuisha chaji na umeme umekata laptom nayo imeisha chaji na unalazimika kukaa masaa mawili kusubiri umeme urudi kwa asilimia kubwa hofu na mhemko unaopitia muda huo ndio unaoitwa FOMO
tunaogopa "missing out" tupo na simu zetu kila mahali hadi unapokwenda uani upo nayo na unaendelea kuperuzi,unaogopa "missing out" tunajiskia vibaya kukaa bila kufanya chochote
Amy anatuambia kwamba watu hao hawaogopi muda wa kukaa peke yao mwandishi ametaja baadhi ya watu katika dini kubwa duniani kama Vile Yesu,Mtume Muhammad,Buddha wote hao walionekana mara nyingi wakipata muda wa kukaa peke yao kwa utulivu
mwandishi anatuambia tuwe na ujasiri wa kukaa peke yetu hata kwa muda mfupi anasema tu "SCHEDULE A DATE WITH YOURSELF" kutafakari kuhusu maendeleo yako ulipofikia na unapoelekea,
10. THEY DON’T FEEL THE WORLD OWES THEM ANYTHING
Tafsiri yake:Hawatarajii ulimwengu kuwapa chochote.
Don’t go around saying the world owes you a living. The world owes you nothing. It was here first. —ROBERT JONES BURDETTE
Hii inaelezea watu ambao wana mtazamo wa unyenyekevu na uhalisia kuhusu maisha. watu wanaofahamu kuwa mafanikio, furaha, na bahati nzuri haviwezi kuhakikishwa au haviwezi kupatikana moja kwa moja. Badala ya kuhisi kuwa wana bahati ya kupata matokeo chanya, wanachukua jukumu la maisha na matendo yao. Hawaulalamikii ulimwengu au watu wengine wakati mambo hayaendi sawa.
mwandishi anasema kwamba mtazamo huo utatuweka katika Matarajio yasiyo ya kweli,Ukosefu wa shukrani: sababu watu wanapohisi wanastahili mambo fulani, wanaweza kushindwa kuthamini juhudi za wengine au thamani ya kile walicho nacho. Hii inaweza kusababisha uhusiano uliojaa misukosuko na ukosefu wa shukrani kwa ujumla.ugumu wa kukabiliana na shida: Hisia za kustahili zinaweza kufanya iwe vigumu kukabiliana na vikwazo, kushindwa, au kukosolewa
moja ya kitu mwandishi anasema ni kwamba kutokuhesabu "dont keep score" ushazoea unahesabu watu waliokusaidia na unategemea kusaidiwa tena hapo baadae ukweli ni kwamba inaweza isiwe hivyo na kama ukiendelea na mtazamo huo utahuzunishwa sana
Unyenyekevu utakufanya uwe imara zaidi
11. THEY DON’T DWELL ON THE PAST & THEY DONT FEAR TAKING CALCULATED RISK
Tafsiri yake:Hawaishi katika mambo yaliyopita
"We do not heal the past by dwelling there; we heal the past by living fully in the present."—MARIANNE WILLIAMSON
mwandishi ameweka wazi kwamba hatuwezi kupona kama tutaendelea kuyaishi yaliyopita
Je unatamani kama ungeweza kugeuza yaliyokupata huko nyuma ? Unatumia muda mwingi kuwaza kwamba kama ninge....."
aina hiyo ya mawazo yatakuzuia kuishi vizuri katika wakati uliopo yatakufanya uhisi kwamba huna unachoweza kukifanya
hivyo unaweza ukachagua kuwekeza zaidi nguvu zako katika wakati uliopo na kama ulielewa pale juu kwenye namba 4 mambo yaliyopita pia yapo nje ya uwezo wako huwezi kurudi na kuyabadilisha tena ila unaweza ukaamua hali yako ya sasa hivi
MWISHO
2 comments
Let us work on them