Kukabiliana na nyakati ngumu

Inawezekana umefikia hatua ngumu maishani. Mambo hayaendi kama ulivyopanga. Unahisi umekwama

Huenda ni katika kazi yako au kwenye uhusiano. au labda unaona una mwaka mbaya. Au hata siku mbaya 

Wakati wowote unapohisi kukata tamaa au kwamba huna bahati au huzuni nyingi, Jaribu hili 

Mtafute mtu anayehitaji msaada—labda mtu ambaye pia anahisi maisha yake hayapo vizuri—na mfanyie jambo. Sio lazima iwe jambo kubwa. Ongea naye ,Mpe kinywaji, shada dogo

au mpigie tu simu kumsalimia  Mtu huyo hata sio lazima awe mtu unayemjua. Nenda kwenye nyumba ya wazee fanya chochote kitu ambacho kinaweza kuwa na msaada kitu ambacho kitawafanya wahisi kwamba kuna watu wanawaona na kuwajali ,hali zao zikiimarika hali yako inaimarika pia

  Mara tu umefanya tendo fulani la fadhili au ukarimu,angalia jinsi unavyohisi baada ya hapo

Je kuna unafuu kidogo? kama sivyo jaribu tena 

Utagundua kwamba kadri unavyowapa wengine, ndivyo unavyozidi kujiskia vizuri zaidi

 Ulichokisoma hapo juu kinaitwa "helper's high" ni ile hali ya kujiskia vizuri baada ya kuwasaidia wengine unaweza kuitumia vizuri mbinu hiyo kukabiliana na nyakati ngumu


  

Health Talks... Welcome to WhatsApp chat
Howdy! How can we help you today?
Type here...